
Mfumo Dume Bado Watajwa Kuwa Kikwazo Wanawake Kushiriki Kwenye Uongozi
Hali hii ya kutokuwepo na uwiano sawa kati ya wanawake na wanaume kwenye nafasi mbalimbali za uongozi imeelezwa na wadau mbalimbali kuwa chimbuko lake ni mfumo dume uliopo licha ya sera, sheria na maazimio mbalimbali ya kimataifa kuhusu usawa wa kijinsia ambayo Tanzania na Zanzibar zimeridhia.