The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on April 20, 2024. Register Here

Search
Close this search box.

Mara. Wasafiri wanaopita barabara ya Musoma-Majita wilaya ya Musoma vijijini wamekwama kwa takribani saa 9 kutokana na maji kujaa kwenye mto Suguti.

Kujaa kwa mto huo kumetokana na mvua zinazoendelea kunyesha mikoa ya Manyara na Arusha ambayo humwaga maji katika mito Mara na Suguti.

Hii siyo mara ya kwanza kwa watumiaji wa barabara hii kukwama kutokana na mto Suguti kujaa pindi mvua zinapokuwa nyingi katika mikoa ya Manyara kupelekea kukatika kwa mawasiliano katika barabara hii.

Wananchi waliokwama katika eneo hilo wanaomba mamlaka inayohusika na barabara ya Musoma-Majita kuangalia sehemu ya daraja la Suguti kwa kuwa ni korofi Ili waweze kupunguza kero Kwa wananchi.

Hali imekuwa ikisababisha nauli kupanda na kutumia gharama kubwa kutafuta njia mbadala.