The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on April 20, 2024. Register Here

Search
Close this search box.

Mtwara. Watu 6 wamefariki na wengine watano wamejeruhiwa baada ya kupigwa na radi wakiwa kwenye sherehe ya kumpongeza kijana wao kuhitimu elimu ya kidato cha nne.

Taarifa ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara Nicodemus Katembo inaeleza kuwa tukio hilo limetokea Disemba 3, 2023 majira ya saa 12 jioni katika kijiji cha Maparagwe kata ya Chikukwe wilayani Masasi.

Aidha taarifa nyingine inaeleza kuwa mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Angelus Mwinyuku mwenye umri wa miaka 49, Mratibu wa Elimu Kata ya Matawale na mkazi wa Jida wilaya ya Masasi amejinyonga mpaka kufa siku ya Disemba 3, 2023, majira ya saa 12 jioni.

Mwinyuku anadaiwa kujinyonga kwa kutumia kamba ya manila ambayo aliifunga kwenye dirisha la bafu la Ofisi ya Chama cha Walimu (CWT) wilaya iliyopo mtaa wa Wapi Wapi.

Jeshi la Polisi mkoani hapa limesema linaendela kufanya uchunguzi kujua chanzo cha tukio hilo kwa kuwa mpaka sasa bado hakijulikana