The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on April 20, 2024. Register Here

Search
Close this search box.

Dodoma. Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU mkoa wa Dodoma imebaini kuwepo kwa mapungufu katika miradi ya maendeleo 28 iliyofanyiwa ufuatiliaji ikiwemo wazabuni kulipwa fedha nyingi nje ya mikataba na kulipwa fedha kabla ya kuwasilisha vifaa.

Haya yameelezwa na Mkuu wa TAKUKURU Dodoma, John Joseph wakati akitoa taarifa ya utendaji katika kipindi cha Julai hadi Septemba, 2023.

“Mapungufu haya yamepelea kufunguliwa kwa majadala ya uchunguzi kwa baadhi ya miradi” amesema Joseph “Aidha, elimu na ushauri umetolewa kwa baadhi ya miradi.”

Mapungufu mengine ya miradi hii ambayo ina thamani ya zaidi ya bilioni 5 ni pamoja na uezekaji wa majengo kwa kutumia mabati yaliyochini ya kiwango, wazabuni kulipwa fedha na kuwasilisha vifaa pungufu, fedha za zuio kukatwa kwa wakandarasi na kutowasilisha katika mamlaka husika