The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on April 20, 2024. Register Here

Mahakama Yawafutia Watatu Mashtaka ya Kudaiwa Kuchoma Ofisi za CCM Oktoba 29

Watuhumiwa hao Mohamed Madea(28), Fredy Chacha(21) na Peter Basoti Chobe (48) wamerudi Mahabusu kwa kuwa bado wana shitaka la uhaini

subscribe to our newsletter!

Dar es Salaam. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewafutia mashtaka watuhumiwa watatu waliokuwa wakikabiliwa na mashtaka ya kuchoma ofisi za CCM huko Kivule Majohe.

Watuhumiwa hao ni Mohamed Madea(28), Fredy Chacha(21) na Peter Basoti Chobe (48).Akizungumza juu ya shauri hilo, Wakili wa watatu hao, Wakili William Maduhu ameeleza kuwa Ofisi ya Mashtaka ilishindwa kuthibitisha madai hayo.

Watuhumiwa hao watatu wamerudi mahabusu kwa kuwa bado wana shauri lingine la uhaini. Wakili William Maduhu ametoa wito kwa Mwendesha Mashtaka kuliondoa shitaka hilo.

“Ni wito wangu ndugu DPP uyaondoe mashtaka hayo ya uhaini kwa sababu kama umeshindwa mashtaka ya uchomaji sina hakika na sina imani kwamba unaweza ukathibitisha mashtaka ya uhaini,” alieleza Wakili Maduhu.

Familia za washtakiwa pia zimetoa wito kwa Mwendesha Mashtaka kuondoa mashtaka yaliyobaki ya uhaini.

“Imeonekana kwamba watoto wetu hawana hatia, kwa kweli tumetaabika sana,” Sheila Mohamed, mzazi wa mmoja wa watuhumiwa anaeleza.

Journalism in its raw form.

The Chanzo is supported by readers like you.

Support The Chanzo and get access to our amazing features.
Digital Freedom and Innovation Day
The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on Saturday April 20, 2024 at Makumbusho ya Taifa.

Register to secure your spot

Did you enjoy this article? Consider supporting us

The Chanzo is supported by readers like you.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Posts

×