The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on April 20, 2024. Register Here

Search
Close this search box.

Mahakama kuu ya Tanzania Kanda ya Mtwara imewahukumu kunyongwa  hadi kufa, Badilu Mussa Hannogi [25] na Salum Ally Mauji [24]  wote wakazi wa Mtwara, baada ya kukutwa na hatia ya kumuua Mohamed Juma Mohamed ambaye alikuwa muendesha bodaboda hapa Mtwara.

Kesi hiyo namba 60/2022 imetolewa hukumu Aprili 15, 2024 na jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mtwara Matha Mpaze.

Kwa mujibu wa mahakama ni kwamba mnamo tarehe Januari 15, 2021 majira ya jioni washtakiwa hao walimkodi marehemu  Mohamed Juma Mohamed awapeleke nyumbani kwao wakitokea maeneo ya Cocobeach Manispaa ya Mtwara Mikindani, wakiwa njiani walianza kumshambulia hadi kumuua na mwili kuutupa porini kisha kuchukua pikipiki yake.

Baada muda, Jeshi la Polisi lilichunguza tukio hilo na kuwakamata Badilu na Salum wakituhumiwa kufanya tukio hilo ambapo Februari 2022, walifikishwa makamani kwa mara ya kwanza.