The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on April 20, 2024. Register Here

Search
Close this search box.

Mahakama Kuu Yatupilia Mbali Pingamizi la Wakazi wa Isela, Songwe Kupinga Kuhamishwa Kupisha Hifadhi

Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya imefutilia mbali shauri namba 41 la mwaka 2023 la wakazi wa Isela kijiji Cha Ndolezi mkoani Songwe dhidi ya serikali na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kutaka kupisha hifadhi ya Kimondo.

subscribe to our newsletter!

Mbeya. Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya imefutilia mbali shauri namba 41 la mwaka 2023 la wakazi wa Isela kijiji Cha Ndolezi mkoani Songwe dhidi ya serikali na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kutaka kupisha hifadhi ya Kimondo.

Hayo yamebainishwa Ijumaa,  Agosti 23, 2024,  jijini Mbeya chini ya  Jaji mkuu Mussa Pomo wakati akisikiliza shauri hilo amesema upande wa wadai hauelezi ukubwa wa eneo linalobishaniwa lakini pia kesi hiyo imefunguliwa na mtu zaidi ya mmoja na kila mtu anamiliki eneo lake ambapo haijaainishwa kwenye hati iliyopo mahakamani hapo kuwa kila mtu anamiliki eneo la ukubwa gani na namba ngapi.

Itakumbukwa kuwa mwaka 2022 wakazi hawa wapatao 120 walitakiwa kuhama katika maeneo yao ili kupisha hifadhi ya Kimondo chini ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, hali iliyopelekea wakazi hawa kufungua shauri katika Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya.

Kwa upande wake wakili Philip Mwakilima ambaye hakuwepo mahakamani hapo akizungumza kwa njia ya simu amesema atakutana na mawakili wenzake upande wa wadai na wananchi ambao wamefungua shauri hilo ili kufahamu hatua zitakazochukuliwa zaidi ikiwemo kukata rufaa.

Digital Freedom and Innovation Day
The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on Saturday April 20, 2024 at Makumbusho ya Taifa.

Register to secure your spot

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *