The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on April 20, 2024. Register Here

Tundu Lissu Akamatwa Mbinga

Tundu Lissu amekamatwa na kupelekwa kituo cha polisi Mbinga pamoja na wanachama wengine wa CHADEMA

subscribe to our newsletter!

Mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu amekamatwa na Jeshi la Polisi, Mbinga mkoani Ruvuma punde baada ya kumaliza mkutano wake leo April 09, 2025.

“Baada ya mkutano leo jioni saa 12:00 wilaya ya Mbinga, wakati wa kufunga mkutano OCD alimfuata Mwenyekiti Tundu Lissu Jukwani akamwambia tafadhali ukishuka hapo jukwani Ingia kwenye gari ya Polisi nakutaka Polisi kwa mahojiano. Mh Lissu alimwambia nimefanya nini ? Huku akiendelea kuchangisha fedha ktk hadhara ‘ Tone Tone,” ameandika Godbless Lema kwenye ukurasa wake wa X.

“Baada ya kuona hiyo zogo , Kamanda Sosopi alimfuata OCD nakumwambia kama Lissu analo jambo na nyie [tafadhali] mnaweza kuja pale tulipofikia mkamchukua kwa utaratibu hapa mtazua tafrani kubwa maana halaiki hapa ni kubwa, pia mimi nilisisitiza ushauri huo kwa OCD na wasaidizi wake wengine, alionekana kama anaelewa lakini ghafla mabomu ya machozi mengi yalianza kurindima. Mh Lissu amekamatwa na sasa yuko kituo cha Polisi Mbinga,” anaeleza zaidi Lema.

Katika taarifa yake, CHADEMA imeeleza wengine waliokamatwa ni pamoja na Aden Mayala, Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Kusini, Felius Festo, Mratibu wa Uhamasishaji BAVICHA Taifa, Shija Shebeshi na mlinzi wa Lissu.

Bado jeshi la Polisi halijatoa taarifa rasmi juu ya sabbau za kumshikilia Lissu.

Journalism in its raw form.

The Chanzo is supported by readers like you.

Support The Chanzo and get access to our amazing features.
Digital Freedom and Innovation Day
The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on Saturday April 20, 2024 at Makumbusho ya Taifa.

Register to secure your spot

Did you enjoy this article? Consider supporting us

The Chanzo is supported by readers like you.

One Response

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Posts

×