The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on April 20, 2024. Register Here

Lissu Apandishwa Kizimbani Shtaka la Uhaini

Hati ya mashtaka inaonesha Lissu anatuhumiwa kosa hilo kutokana na maneno aliyoyasema mnamo April 03, 2025,

subscribe to our newsletter!

Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu amefikishwa katika Mahakama ya Kisutu na kusomewa shitaka la uhaini katika moja ya kesi iliyotajwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Kisutu.

“Kwa kuwa Mahakama hii ya Hakimu Mkazi wa Kisutu haina mamlaka hayo, kwa sababu kesi hiyo inatakiwa isikilizwe na Mahakama Kuu basi suala hilo limetajwa na kwa kuwa Mahakama haina mamlaka na kosa hio halina dhamana, Mwenyekiti wa CHADEMA ndugu Lissu hajapata dhamana na hakuweza kusema lolote kuhusiana na mashtaka hayo,” ameeleza Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, Wakili Rugemeleza Nshala.

Hati ya mashtaka inaonesha Lissu anatuhumiwa kosa hilo kutokana na maneno aliyoyasema mnamo April 03, 2025, akiongea na watia nia wa CHADEMA juu ya kampeni ya chama hicho ya ‘bila mageuzi, hakuna uchaguzi’.

Kesi ya uhaini ni moja ya kesi yenye adhabu ya juu kabisa ambayo ni kifo, kesi ya kwanza ya uhaini ni ile ya mwaka 1969, iliyowahusisha baadhi ya wapigania uhuru akiwemo Bibi Titi Mohamed ambapo alishitakiwa pamoja na watuhumiwa wengine akiwemo mwandishi Gray Likungu Mattaka, John Dunstan Chipaka, Eliyah Lifa Chipaka, Michael Kamaliza na William Magori Chacha.

Katika kesi nyingine, Tundu Lissu pia ameshtakiwa kwa makosa ya kuchapisha taarifa za uongo.

Journalism in its raw form.

The Chanzo is supported by readers like you.

Support The Chanzo and get access to our amazing features.
Digital Freedom and Innovation Day
The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on Saturday April 20, 2024 at Makumbusho ya Taifa.

Register to secure your spot

Did you enjoy this article? Consider supporting us

The Chanzo is supported by readers like you.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Posts

×