The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on April 20, 2024. Register Here

Watanzania Wawachangia CHADEMA Milioni 105. CHADEMA Wasisitiza Vuguvugu la ‘No-reform’ Sio Uasi

Golugwa amefafanua zaidi kuwa michango hiyo imetumika kuendesha mikutano waliyoipanga kusini

subscribe to our newsletter!

Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Amani Golugwa ametoa tathimini ya michango wanayoendelea kuipokea kutoka kwa Watanzania kupitia njia mbalimbali ambapo katika kipindi cha mwezi uliopita wamekusanya Milioni 105. za michango.

Golugwa ameeleza haya akiongea waandishi wa habari leo Aprili 11, 2025, katika ofisi za chama hicho Mikocheni jijini Dar es Salaam. Michango hiyo imekusanywa kupitia benki ya NMB, kiasi cha Sh. 19,717,971; M-PESA (0744 446 969) kiasi cha Sh. 71,487,831; MPESA Digital kiasi cha Sh. 11,300,000; Airtel Sh. 1,633,343 na CRDB Sh. 928,490.

“Tunajisikia Fahari, tunajisikia heshima, tunajisikia kuwajibika kwa watu ambao wanakiongoza chama chao,” ameeleza Amani Golugwa.

Golugwa amefafanua zaidi kuwa michango hiyo imetumika kuendesha mikutano waliyoipanga katika kanda ya Nyasa na Kusini. Chama hicho kimeeleza pia kimepokea michango ya mali ikiwemo mafuta, chakula na malazi kila walipopita.

Golugwa amegusia pia kuhusu kampeni ya, ‘hakuna mageuzi, hakuna uchaguzi’ kuwa sio uasi.

‘Tunahitaji kuyatatua matatizo na dosari za uchaguzi ambazo wote tunaamini kuna mahali patafikia kikomo, wananchi hawataweza kuvumilia tena, hata wanasiasa hawataweza kuvumilia tena.”

Journalism in its raw form.

The Chanzo is supported by readers like you.

Support The Chanzo and get access to our amazing features.
Digital Freedom and Innovation Day
The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on Saturday April 20, 2024 at Makumbusho ya Taifa.

Register to secure your spot

Did you enjoy this article? Consider supporting us

The Chanzo is supported by readers like you.

One Response

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Posts

×