The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on April 20, 2024. Register Here

Tanzania: Kumekuwepo na Tishio la Kiusalama Linalotokana na Mgogoro wa Mpaka Kati ya Tanzania na Uganda

Tanzania imeeleza kuwa kumekuwepo na tishio la kiusalama katika mpaka wa Tanzania na Uganda kutokana na mgogoro wa kimpaka.

subscribe to our newsletter!

Katika taarifa ya hali ya ulinzi na usalama wa mipaka ya nchi iliyowasilishwa katika taarifa ya bajeti ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa ya mwaka 2025/26 leo Mei 20, 2025, Tanzania imeeleza kuwa kumekuwepo na tishio la kiusalama katika mpaka wa Tanzania na Uganda kutokana na mgogoro wa kimpaka.

“Hali ya usalama katika mpaka huu wenye urefu wa kilomita 397.8 ni shwari. Hakuna tukio la kuhatarisha usalama wa nchi yetu,” ilieleza ripoti hiyo ya Wizara.

“Pamoja na hali hii, kumekuwepo na tishio la kiusalama linalotokana na Mgogoro wa mpaka kati ya Tanzania na Uganda. Pamoja na jitihada za kumaliza mgogoro huu, bado serikali ya Uganda inaendelea kudai kuwa mpaka wake na Tanzania katika eneo la Kagera unapita katika 01° kusini mwa ikweta badala ya marundo ya mawe yaliyopo,” taarifa hiyo inaeleza.

Wizara ilieleza zaidi kuwa mazungumzo yanaendelea chini ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Journalism in its raw form.

The Chanzo is supported by readers like you.

Support The Chanzo and get access to our amazing features.
Digital Freedom and Innovation Day
The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on Saturday April 20, 2024 at Makumbusho ya Taifa.

Register to secure your spot

Did you enjoy this article? Consider supporting us

The Chanzo is supported by readers like you.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Posts

×