The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on April 20, 2024. Register Here

Waumini 52 wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Wafungua Kesi ya Kikatiba Kudai Uhuru wa Kuabudu

Kesi hiyo ya Kikatiba iliyofunguliwa dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Mkuu wa Jeshi la Polisi inategemewa kusikilizwa kesho Julai 11, 2025

subscribe to our newsletter!

Wuamini 52 wa Kanisa la Glory of Christ Tanzania Church, maarufu kama Ufufuo na Uzima wamefungua kesi ya Kikatiba kudai haki yao ya Uhuru wa Kuabudu.

Kesi hiyo ya Kikatiba iliyofunguliwa dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Mkuu wa Jeshi la Polisi inategemewa kusikilizwa kesho Julai 11, 2025, mbele ya Majaji watatu: Jaji Ephery Sedekia Kisanya, Jaji Cyprian Phocas Mkeha na Jaji Zahra Abdallah Maruma. Kesi imesajiliwa kwa namba16408/2025 na imepangwa kusikilizwa majira ya nane na nusu mchana.

Kanisa la Ufufuo na Uzima linalongozwa na Askofu Josephat Gwajima lilufungwa mnamo Juni 02, 2025, kwa kile ambacho barua kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ilieleza kiongozi wa kanisa hilo amekua akitoa mahubiri yenye nia ya kuichonganisha serikali na wananchi.

Kufungiwa kwa kanisa hilo kunafuatia mahubiri na mkutano na waandishi wa habari aliofanya kiongozi wa kanisa hilo kukemea matukio ya watu kutekwa, kupotezwa na kuuwawa, ambapo alizungumza mnamo Mei 24, 2025 na pia mnamo Juni 01, 2025, ambapo alitangaza maombi ya siku saba juu ya masuala hayo.

Kanisa hilo lilingia katika juhudi mbalimbali za kisheria ikiwemo kukataa rufaa, na kupeleka shauri Mahakamani, sehemu zote juhudi hizi hazijafanikiwa kuleta ufumbuzi.

Kesi ilivyopelekwa Mahakamani na kusikilizwa chini ya jaji Juliana Masabo, Mahakama haikuweza kutoa uamuzi wa moja kwa moja katika suala hilo. Hii ni kutokana na kuwa barua ya kulifungia kanisa hilo iliandikwa jina tofauti yaani Glory of Christ Church badala ya Glory of Christ Tanzania Church. Hata mawakili wa serikali waliieleza Mahakama katika shauri hilo kuwa hakuna barua ya kulifungia kanisa la Glory of Christ Tanzania Church na kusisitiza haipo na ni uzushi.

Kanisa hilo pia limefanya juhudi za kukata rufaa kupitia taratibu za kiserikali, yaani kwa Waziri wa Mambo ya Ndani, hata hivyo, Wakili wa Kanisa hilo, Peter Kibatala, alieleza kuwa walipokea barua kutoka kwa Waziri ya Mambo ya Ndani iliyoeleza kuwa hawaitambui barua hiyo ya kulifunguia kanisa hilo.Hata hivyo, barua rasmi ya kukusudia kufuta usajili wa bodi ya wadhamini wa kanisa hilo, tofauti na iliyosambaa mtandaoni, iliweza kuwasilishwa kwa Bodi ya Wadhamini wa Kanisa hilo ikionesha kuwa ilitolewa Juni 03, 2025.

 Inategemewa hapo kesho Julai 11, 2025, Jaji Masabo pia atatoa uamuzi kuhusu huu mkanganyiko baada ya Wakili wa Kanisa hilo kuwasilisha vielelezo vipya.

Toka kanisa hilo lilivyofungwa mnamo Juni 02, 2025, waumini wamekuwa wakijitokeza kwa ajili ya kusali nje ya kanisa kuu lililopo Ubungo Kibo, hata hivyo waumini hao wamejikuta wakiambulia madhila mbalimbali ikiwemo vipigo, na kukamatwa.

Majina ya waleta maombi hao ni pamoja na:

  1. Dinali Mbaga
  2. Elisha Musa
  3. Nsajigwa Lwijisho
  4. Basil Kashumba
  5. Filbert Benedicto
  6. Stephano Samson
  7. Ela Mtishbi
  8. Masihi Kalokola
  9. John Job
  10. Emmanuel Asilia
  11. Joseph John
  12. Augustin Stamili
  13. Lameck Msude
  14. Boniface Maingu
  15. Amani Sahodi
  16. Adoph Makumba
  17. Oscar John
  18. John Fredrick
  19. Erick Michael
  20. Daniel Makiungile
  21. Ozeniel Shelukindo
  22. Wiliriki Kereti
  23. Freeman Kalinga
  24. George Gilbert
  25. Petro Faida
  26. John Boenge
  27. Joseph Fabian
  28. Leopodius Martin
  29. Patrick Augustino
  30. Jacob Silas
  31. Andrew Kamulei
  32. Gwandumi Ngalawa
  33. Beatus Poryton
  34. Amos Makaa
  35. Anderson Hassan
  36. Fanuel Lameck
  37. Bahati Mwampamba
  38. Joshua Musa
  39. Samuel Bernad
  40. Gergina Mwiza
  41. Levina Zakaria
  42. Maria Gidion
  43. Rose Erasto
  44. Nosyaga Mwakila
  45. Janeth Shoo
  46. Anna Meataa
  47. Telesia Michael
  48. Veronica Mbevu
  49. Rhoda Raphael
  50. Laika Mboya
  51. Hilaria Godfrey
  52. Mage Henry

Journalism in its raw form.

The Chanzo is supported by readers like you.

Support The Chanzo and get access to our amazing features.
Digital Freedom and Innovation Day
The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on Saturday April 20, 2024 at Makumbusho ya Taifa.

Register to secure your spot

Did you enjoy this article? Consider supporting us

The Chanzo is supported by readers like you.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Posts

×
×