The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on April 20, 2024. Register Here

Majaliwa Kukosa Kushiriki Kikao cha Uteuzi Watia Nia CCM Akianza Ziara Grenada

Majaliwa hakuweza kushiriki Mkitano Mikuu miwili ya CCM kutokana na ziara za kikazi

subscribe to our newsletter!

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewasili mjini St George, katika visiwa vya Grenada jana Julai 27, 2025, ambapo anategemewa kushiriki katika Jukwaa la nne la Kibiashara na Uwekezaji kati ya Afrika na Karibiani litakalofanyika kuanzia Julai 28 na kumalizika Julai 30.

Hii inamaanisha Majaliwa atakosa kushiriki kikao cha uteuzi cha watia nia wa nafasi za Ubunge CCM, ambapo, yeye ni mmoja wa wajumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho.

Majaliwa pia hakuonekana kuungana na viongozi wenzake waandamizi katika Mkutano Mkuu uliofanyika Julai 26, 2025, kwa njia ya mtandao ambapo viongozi waandamizi wa CCM walikutana  katika ukumbi wa mkutano wa NEC (White House) Makao Makuu ya CCM, Jijini Dodoma.

Katika Mkutano Mkuu wa mwezi Mei 2025, taarifa ya utekelezaji wa ilani 2020-2025, iliwasilishwa na Naibu Waziri Mkuu Doto Mashaka Biteko, kwani Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alikuwa kwenye ziara ya kikazi nchini Japan.

Majaliwa alitangaza kubadili mawazo ya kugombea katika jimbo la Ruangwa katika siku ya mwisho ya uchukuaji fomu za uteuzi mnamo Julai 02, 2025, ambapo alieleza kuwa mabadiliko ni jambo la kawaida.

Journalism in its raw form.

The Chanzo is supported by readers like you.

Support The Chanzo and get access to our amazing features.
Digital Freedom and Innovation Day
The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on Saturday April 20, 2024 at Makumbusho ya Taifa.

Register to secure your spot

Did you enjoy this article? Consider supporting us

The Chanzo is supported by readers like you.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Posts

×
×