The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on April 20, 2024. Register Here

Panga la Kamati Kuu CCM Lawashukia Wabunge Zaidi ya 40. Hawataonekana Kwenye Kura za Maoni CCM

Wabunge zaidi ya 40 ambao wako Bungeni kwa sasa hawataonekana katika kura za maoni ya chama hicho, baadhi ya majina yaliyokumbwa na panga hilo yameendelea kuzua gumzo kubwa mitandaoni.

subscribe to our newsletter!

Shamra shamra za uchaguzi ndani ya Chama cha Mapinduzi zinaendelea, ambapo hivi leo Julai 29, 2025, majina ya watia nia walioteuliwa na Kamati Kuu ya chama hicho kwa ajili ya kwenda kwenye kura za maoni yametangazwa.

Hata hivyo, wabunge zaidi ya 40 ambao wako Bungeni kwa sasa hawataonekana katika kura za maoni ya chama hicho baada ya Kamati Kuu ya chama hicho kuyaondosha. Baadhi ya majina yaliyokumbwa na panga hilo yameendelea kuzua gumzo kubwa mitandaoni.

Mbunge wa Kisesa Luhaga Mpina, ni jina ambalo wengi walikuwa wakisubiria kuona kama atatokea au la, hii ni kutokana na misimamo yake iliyomfanya kuwa maarufu jimboni kwake na miongoni mwa watu wengi, huku akigeuka kuwa mwiba kwa serikali . Jina la Mpina halijarudi na halitakuwepo kati ya watu saba waliopitishwa kama wagombea wa kura za maoni Kisesa.

Akiongea na The Chanzo kuhusu suala hilo Mpina ameeleza kuwa, hana kitu cha kusema kwa sasa kwani ndio amepokea tu taarifa hizo.

Jina lingine lililozua gumzo kubwa ni  la Januari Makamba, Mbunge wa Bumbuli, naye jina lake halitakuwa kati ya majina sita yaliyorudishwa Kwenda kwenye kura za maoni jimboni, wengi  wanahusisha kukatwa kwa jina la Makamba na makundi mbalimbali yaliyoibuka ndani ya chama hicho.

Mbunge wa Arusha, Mrisho Gambo, ambaye amekuwa katika mvutano mkali na Paul Makonda, naye ni moja kati ya watu walioachwa nje ya kinyang’anyiro hicho.

Wengine waliokatwa ni pamoja na Mbunge wa Ngorongoro Emmanuel  Ole  Shangai na Mbunge wa Simanjiro Christopher Ole Sendeka, Wabunge wanaotokea kwenye maeneo ambapo kumekuwepo na mvutano mkali kati ya hifadhi, serikali na jamii hasa za wamasai.

Wabunge wengine ambao nao hawataonekana kwenye kura za maoni ni pamoja na:

  1. Godwin Emmanuel Kunambi, Mbunge wa Mlimba
  2. Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula, Mbunge Ilemela
  3. Twaha Ally Mpembenwe, Mbunge wa Kibiti
  4. Vedastus Mathayo Manyinyi, Mbunge Musoma Mjini
  5. Zuberi Mohamedi Kuchauka, Mbunge wa Liwale
  6. Dr. Alfred James Kimea, Mbunge wa Korogwe Mjini
  7. Rashid  Abdalla     Rashid, Mbunge wa Kiwani
  8. Geoffrey  Idelphonce Mwambe, Mbunge wa Masasi Mjini
  9. Stephen Byabato, Mbunge wa Bukoba Mjini
  10. Abdallah  Jafari  Chaurembo, Mbunge wa Mbagala
  11. Khamis  Said Gulamali, Mbunge wa Manonga
  12. George  Ranwell  Mwenisongole, Mbunge wa Mbozi
  13. Nicodemas  Henry Maganga, Mbunge wa Mbogwe
  14. Hassan  Zidadu Kungu, Mbunge wa Tunduru Kaskazini
  15. Daimu   Iddi Mpakate, Mbunge wa Tunduru Kusini
  16. Mansoor Shanif Jamal, Mbunge wa Kwimba
  17. Justin  Lazaro Nyamoga, Mbunge wa Kilolo
  18. Shabani Omari Shekilindi, Mbunge wa Lushoto
  19. Mohamed Lujuo Monni, Mbunge wa Chemba
  20. Flatei Massay, Mbunge Mbulu Vijijini
  21. Innocent Edward Kalogeris, Mbunge Morogoro Kusini
  22. Ndaisaba  George Ruhoro, Mbunge Ngara
  23. Cecil David Mwambe, Mbunge Ndanda
  24. Toufiq Salim  Turky, Mbunge wa Mpendae
  25. Ravia Idarus Faina, Mbunge wa Makunduchi
  26. Yahya Ali Khamis, Mbunge wa Kijini
  27. Omar Ali Omar, Mbunge wa Wete
  28. Juma Hamad Omar, Mbunge wa Ole
  29. Haji Makame Mlenge, Mbunge wa Chwaka
  30. Simai Sadiki, Mbunge wa Nungwi
  31. Ahmed Ngwali, Mbunge wa Ziwani
  32. Abbas Ali Mwinyi, Mbunge wa Fuoni
  33. Amour Khamis Mbarouk, Mbunge wa Tumbe
  34. Omar Issa Kombo, Mbunge wa Wingwi
  35. Khamis Hamza Khamis, Mbunge wa Uzini
  36. Salum Mohammed Shaafi, Mbunge wa Chonga
  37. Iddi Kassim Iddi, Mbunge wa Msalala

Journalism in its raw form.

The Chanzo is supported by readers like you.

Support The Chanzo and get access to our amazing features.
Digital Freedom and Innovation Day
The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on Saturday April 20, 2024 at Makumbusho ya Taifa.

Register to secure your spot

Did you enjoy this article? Consider supporting us

The Chanzo is supported by readers like you.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Posts

×
×