The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on April 20, 2024. Register Here

Msigwa: Watumishi wa Umma Wafanyie Kazi Nyumbani Kasoro Wenye Majukumu ya Kazi Yanayowataka Kuwepo Eneo la Kazi

Katika taarifa ya Msigwa ambayo imetoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi na kuchapwa kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram amesema uamuzi huo ni kufuatia angalizo la kiusalama lililotolewa na Jeshi la Polisi kwa wakazi wa Dar es Salaam.

subscribe to our newsletter!

Msemaji Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Gerson Msigwa ametoa taarifa kuwa watumishi wote wa umma nchini Tanzania kufanyia kazi nyumbani siku ya Oktoba 30, 2025 isipokuwa wale ambao majukumu yao yanawahitaji kuwepo eneo la kazi.

Katika taarifa ya Msigwa ambayo imetoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi na kuchapwa kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram amesema uamuzi huo ni kufuatia angalizo la kiusalama lililotolewa na Jeshi la Polisi kwa wakazi wa Dar es Salaam.

“Aidha, waajiri katika Sekta Binafsi wanashauriwa kuzingatia tahadhari hiyo na kuwaruhusu watumishi wao nao kufanya kazi nyumbani,” imeeleza taarifa hiyo.

Imeeleza pia wananchi wasio na ulazima wa kutoka kwenye makazi yao wanashauriwa  kufanyia shughuli zao nyumbani.

Oktoba 29, 2025 jioni mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania IJP Camillus Wambura alitoa amri kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam kutotoka nje kuanzia saa 12 jioni, kama angalizo kufuatia vurugu kuripotiwa kwenye baadhi ya maeneo ya jiji la Dar es Salaam siku ya zoezi la kupiga kura.

Ripoti mbalimbali zinaonesha kuwa yamefanyika maandamano maeneo mbalimbali ya Dar es Salaam na baadhi ya maeneo ya mikoa ya Mbeya, Arusha, Songwe na Shinyanga. 

Journalism in its raw form.

The Chanzo is supported by readers like you.

Support The Chanzo and get access to our amazing features.
Digital Freedom and Innovation Day
The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on Saturday April 20, 2024 at Makumbusho ya Taifa.

Register to secure your spot

Did you enjoy this article? Consider supporting us

The Chanzo is supported by readers like you.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Posts

×