
Kampeni Maalum Yazinduliwa Kuhamasisha Ujenzi wa Vituo vya Huduma za Utambuzi na Upimaji wa Mahitaji Maalum ya Ujifunzaji wa Watoto
Kampeni hiyo imeandaliwa na shirika la HakiElimu kwa kushirikiana na Child Support Tanzania (CST), ikiwa na lengo la kuhamasisha halmashauri pamoja na Serikali Kuu kuwekeza zaidi katika huduma za utambuzi wa awali kwa watoto wenye changamoto za ujifunzaji na maendeleo.


