The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on April 20, 2024. Register Here

Waliokuwa Wakuu wa Mikoa, Wilaya, Wakurugenzi Sasa Rasmi Kwenye Kipute cha Kura za Maoni CCM Baada ya Mkeka Mpya wa Uteuzi Kutoka

Wataeule hao walitakiwa kuandika rasmi kuonesha nia zao za kuingia kwenye uchaguzi ujao.

subscribe to our newsletter!

Mkeka mpya wa wateule wapya wa Rais katika nafasi za wakuu wa wa mkoa, wilaya na wakurugenzi umetoka rasmi Juni 23, 2025, hii ikimaanisha baadhi ya wateule walioonesha nia ya kwenda majimboni kugombea kupitia Chama cha Mapinduzi wanaingia rasmi kwenye mchuano wa kura za maoni.

Wateule hao walitakiwa kuandika rasmi kuonesha nia zao za kuingia kwenye uchaguzi ujao. Uchaguzi huu unatarajiwa kuwa wa kipekee katika historia ya Tanzania baada ya chama kikuu cha upinzani nchini, CHADEMA, kutangazwa kuzuiwa rasmi kushiriki katika uchaguzi na Tume ya Taifa ya Uchaguzi mnamo Aprili 12, 2025.

Mnamo Machi 11, 2025, katika mkutano wa 39 wa Jumuiya za Serikali za Mtaa (ALAT), Rais Samia alitoa wito kwa wale walioshika nafasi mbalimbali za serikali na wana nia ya kugombea watoe taaarifa rasmi serikalini.

“Nilimuambia Katibu Mkuu kiongozi peleka waraka rasmi Serikali za Mitaa. Yeyote mwenye nia ya kugombea atuambie mapema ili tumpandishe wa chini yake ashike ile nafasi. Hatutaki pale tayari fomu zinatoka watu wote wanakimbia kwenda kuchukua fomu mnatuacha Serikali za Mitaa hazina viongozi, hazina wasimamizi. Mnabakia kujaza watu ambao hawana uzoefu. Lakini tukijua mapema tutatayarisha watu wa kujaza hizo nafasi,” alieleza Rais Samia.

“Sasa usipojisema mapema, ukija ukichukua fomu mbele umekosa yote. Umekosa fomu, umekosa cheo, nafasi yako utaiacha. Ukituambia mapema, ukituambia mapema, umekwenda kujaribu, umeshindwa na wewe ni mzuri tutakufikiria kurudi,” alisisitiza zaidi Rais Samia.

Baadhi ya mabadiliko yaliyofanyika ni pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Kenan Leban Kihongosi, kuhamishiwa Arusha kurithi mikoba ya Paul Makonda. Tetesi mbalimbali zinaonesha Makonda anatarajiwa kuingia kwenye kura za maoni Arusha. Mpaka sasa amekuwa na mvutano mkali na Mbunge wa sasa wa Arusha, Mrisho Gambo. Anamringi Macha amehamishwa kutoka kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga na kwa sasa atahamia rasmi Simiyu kama Mkuu wa Mkoa mpya.

Wengine walioteuliwa ni pamoja na Mkuu wa Jeshi la Polisi Mstaafu, Balozi Simon Sirro ambaye amekuwa Mkuu wa Mkoa wa Kigoma akichukua nafasi ya Thobias Andengenye. Kheri James, aliyekuwa Mkuu wa Wilaya Iringa amepandishwa na kuwa Mkuu wa Mkoa Iringa akichukua nafasi ya Peter Serukamba, aliyetangaza mapema mwezi wa tano nia yake ya kugombea Ubunge.

Mboni Mohamed Mhita aliyekuwa Mkuu wa Wilaya Kahama ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga. Beno Malisa aliyekuwa Mkuu wa Wilaya Mbeya pia ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya akichukua nafasi aliyokuwa ameishika Juma Zuberi Homera, ambaye katika ukurasa wake wa Instagram, ameonesha kuwa anaenda kugombea Ubunge; “Tayari ule Muda umefika, tukutane site 2025,” anaandika Homera.

Jabiri Omari Makame ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Songwe, nafasi iliyokuwa ikishikiliwa na Daniel Godfre Chongolo. Katika ukurasa wake wa Instagram Chongolo ameeleza kuwa anarudi Njombe: “Kijiti nakikabidhi kwa mdogo wangu mkubwa Jabir makame…narudi nyumbani Njombe,” ameeleza Chongolo.

Aliyekuwa Mkurugenzi wa Shirika la Reli, Masanja Kadogosa naye ameondolewa kwenye nafasi aliyokuwa anaishikilia na Injinia Machibya Masanja kuteuliwa, Machibya alikua ni Mkurugenzi wa miundombinu katika Shirika la Reli. Kadogosa amekuwa akitajwa tajwa Bariadi, na hata katika ziara ya Katibu Mkuu wa CCM, Emmanuel Nchimbi mnamo Juni 15, 2025, Kadogosa alisimamishwa pamoja na Mbunge wa sasa, Kundo Andrea Mathew na Mbunge wa Viti Maalum Lucy Sabu, ambapo Katibu wa chama hicho alisisitiza kuwa chama hicho kinawahitaji wote, akiongelea kuhusu suala la uchaguzi ndani ya chama hicho.

Mabadiliko haya yanakuja katika siku hiyo hiyo ambayo CCM imetangaza kusitisha ziara, mikutano, semina na makongamano, yanayohusisha wajumbe wa vikao vinavyopigia kura za maoni hadi baada ya kura za maoni, ikionekana ni jitihada za kuzuia ushawishi usio halali kwa wajumbe, Katikati ya joto kali la mchakato wa kura za maoni.

Wengine walioteuliwa jana Juni 23, 2025, ni pamoja na:

  1. Bi. Agnes Meena ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi.
  2. Bw. Rashid Kassim Mchata amehamishwa kutoka Mkoa wa Pwani kwenda kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga
  3. Bi. Pili Hassan Mnyema amehamishwa kutoka Mkoa wa Tanga kwenda kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani.
  4. Bw. Abdul Rajab Mhinte ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam
  5. Dr. Frank Hawasi ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe.\
  6. Dr. Hussein Mohamed Omar amehamishwa kutoka Wizara ya Kilimo kwenda kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
  7. Prof. Peter Lawrence Makenga Msoffe ameteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia masuala ya mazingira
  8. Mhandisi Athumani Juma Kilundumya ameteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Kilimo anayeshughulikia masuala ya maendeleo ya mazao na usalama wa chakula
  9. Solomon Jonas Itunda amehamishwa kutoka Wilaya ya Songwe kwenda kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mbeya
  10. Japhari Kubecha Mghamba amehamishwa kutoka Wilaya ya Handeni kwenda kuwa Mkuu wa Wilaya ya Gairo
  11. Amir Mohamed Mkalipa amehamishwa kutoka Wilaya ya Arumeru kwenda kuwa Mkuu wa Wilaya ya llemela
  12. Estomin Mwatuyobe Kyando ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kilolo
  13. Ayubu Yasin Sebabile ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Muheza
  14.  Thecla Mkuchika ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Butiama
  15. Angelina Marco Lubela ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Serengeti
  16. Maulid Hassan Dotto ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mvomero
  17. Rukia Ally Zuberi ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mwanga
  18. Mwinyi Ahmed Mwinyi ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Arumeru
  19. Jubilete Win Lauwo ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Magu
  20. Mikaya Tumaini Dalmia ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni
  21. Thomas Mendraid Myinga ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Sikonge
  22. Gloriana Julius Kimath ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Monduli
  23. Upendo Bert Wella ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Tabora
  24.  Denis Gervas Masanja ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Tunduru
  25. Fadhil Emanuel Nkurlu ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Songwe
  26. Benjamin Samwel Sitta ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Iringa
  27. Salum Nyamwese ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Handeni
  28. Frank John Mkinda ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kahama
  29. Mwanamwaya Kombo ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Mkinga
  30. Kassim Salum Kirondomara ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Biharamulo
  31. Thobias Abwaro ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Babati
  32. Asycritus Mumena Egaruk ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Meatu
  33. Nyakaji Etanga Mashauri ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Kilolo
  34. Mustapha Ayubu Kimomwe ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Rufiji
  35. Milama Masiko ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Serengeti
  36. Mpampalika Mfaume Mpampalika ameteuliwa kuwa Katibu Tawala Wilaya ya Mwanga
  37. Richard Jackson Mwalingo ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Mtwara
  38. Zuberi Said Zuberi ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Magu
  39. Angela Henry Mono ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Tanga
  40. Mamndolwa Miraj Gembe ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Same
  41. Sabina Starlin Mwajeka ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Momba
  42. Sosthenes Chakupanyuka ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Kaliua
  43. Adestino Gwelino Mwilinge ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Mbogwe
  44. Justice Laurent Kijazi amehamishwa kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Iringa kwenda kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya
  45.  Zaina Mfaume Mlawa amehamishwa kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Bahi kwenda kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa
  46. Raymond Mweli ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali
  47. Adelina Enock Mfikwa ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
  48. Iddi Ally Ndabona ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi
  49. Hamisi Hamidu Idd ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega
  50. Mwarami Seif ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
  51. Bi. Newaho Mkisi ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  52. Zainab Salum Mgomi ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Nanyamba
  53.  John Marco Pima ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
  54.  Albina Willium Mtumbuka ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
  55. Paulo Francis Faty ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero
  56. Shabani Kabelwa ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
  57. Vicent Augustino Mbua ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe.

Journalism in its raw form.

The Chanzo is supported by readers like you.

Support The Chanzo and get access to our amazing features.
Digital Freedom and Innovation Day
The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on Saturday April 20, 2024 at Makumbusho ya Taifa.

Register to secure your spot

Did you enjoy this article? Consider supporting us

The Chanzo is supported by readers like you.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Posts

×