The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on April 20, 2024. Register Here

Kanisa Katoliki Tanzania Lapiga Marufuku Mapadri, Watawa Kushiriki Kampeni za Siasa. Ni Siku Moja Baada ya Masista Kupigwa Picha Kwenye Kampeni

Tamko hili linakuja ikiwa siku moja baada ya picha iliyosambaa ikiwaonesha Masista wa kituo cha Masista wa Mtakatifu Benedicto wa Msaada wa Kikristo Afrika kutoka Ndanda

subscribe to our newsletter!

Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, Wolfgang Pisa, ametangaza marufuku juu ya watumishi wa kanisa hilo kushiriki katika kampeni za siasa. Akiongea  leo Septemba 25, 2025, katika misa ya kuadhimisha miaka mia moja ya seminari ya Kipalapala-Tabora, Pisa ameeleza marufuku hiyo ipo kwa mujibu wa kanuni za Kanisa hilo lenye miaka 2000 duniani.

“Mtawa, Padri au kiongozi yeyote wa kanisa hapaswi kushiriki katika kampeni zozote za siasa. Wala hapaswi kutambulishwa na chama chochote kwa kuvalishwa gwanda lolote la chama chochote cha siasa au kiashiria chochote. Ni Marufuku Mapadri, marufuku kwa watawa, marufuku kwenu nyinyi waseminaristi kuonekana kwenye kampeni ya siasa, marufuku kubwa,” alieleza Askofu Pisa.

Tamko hili linakuja ikiwa siku moja baada ya picha iliyosambaa ikiwaonesha Masista wa kituo cha Masista wa Mtakatifu Benedicto wa Msaada wa Kikristo Afrika kutoka Ndanda, wakionekana katika mkutano wa kampeni wa Chama Cha Mapinduzi, huko Masasi, Mtwara wakiwa wameshikilia machapisho mbalimbali ya kampeni.

Masista wa Mtakatifu Benedicto wa Msaada wa Kikristo Afrika, Ndanda, katika mkutano wa kampeni za CCM, Masasi| Septemba 24, 2025

Katika hotuba yake Pisa ameonya juu ya kuvaa mavazi kama kofia au T-sheti za vyama vya siasa. Na kuwasihi wadau wa siasa kusubiri muda wa kupiga kura ikiwa wanaamini kuna wafuasi wao miongoni mwa watumishi wa kanisa hilo.

“Na ni vibaya watu kurubuni na kuhadaa watu, hao wahusika wakipita kwenye nyumba za kanisa, wakipita kwenye convet za kanisa kuwahadaa na kuwarubuni hiyo ni dhambi haipaswi,” alieleza Pisa.

“Haipaswi kumrubuni mtu kitu ambacho hafahamu, unamkamata Mnovisi, unamkamata Mtawa mmoja Mklara ambaye hata redio hasikilizi, taarifa ya Habari hasomi, unamsomba tu, halafu unamuelekeza, unamfanyisha ile doctrination, hiyo ni dhambi na ni makosa makubwa, marufuku,” alisisitiza zaidi.

Journalism in its raw form.

The Chanzo is supported by readers like you.

Support The Chanzo and get access to our amazing features.
Digital Freedom and Innovation Day
The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on Saturday April 20, 2024 at Makumbusho ya Taifa.

Register to secure your spot

Did you enjoy this article? Consider supporting us

The Chanzo is supported by readers like you.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Posts

×