Wadau Wamshukia Makalla Kwa Madai Yake Kuwa CHADEMA inapanga Kusambaza Virusi vya Ebola Kuzuia Uchaguzi: ‘Maneno ya Hovyo’
Amos Makalla, Katibu wa Itikadi, Uenezi, na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), yuko matatani kwa kudai kwamba chama cha upinzani, CHADEMA, kinakusanya fedha ili ‘kikanunue’ virusi vya Mpox na Ebola kwa ajili ya shambulio la kibaiolojia ili kuvuruga uchaguzi nchini.