Kuachiwa kwa Mbowe na Mapungufu ya Mfumo wa Utoaji Haki Tanzania
DPP, kama mfumo wa utoaji haki Tanzania ungekuwa mzuri, angeweza kusema kwamba katika kupitia upya ushahidi uliokusanywa kuhusu shauri husika, anaona, pasipo shaka yoyote, kuwa watuhumiwa hawawezi kutiwa hatiani na hivyo anaona kuwa ni kupoteza muda wa Jamhuri na watuhumiwa kuendelea na shauri husika.