
Panga la Wajumbe CCM Lilivyowashughulikia Wabunge, Naibu Mawaziri. Kazi Imebaki Vikao vya Mchujo Baada ya Kura ya Maoni
Katika wabunge walioangukia pua katika mchakato huo wa kura za maoni, wapo wabunge wakongwe waliokaa bungeni kwa zaidi ya miaka 20, lakini pia wapo wabunge ambao wamehudumu kwa kipindi cha muhula mmoja tu. Lakini kubwa zaidi ni zaidi ya Naibu Mawaziri saba wameangushwa na kuachwa mbali kwa kura kwenye majimbo yao.








