
January Makamba Akanusha Kuengulia Sababu ya Mbio za Urais, Atuma Salamu kwa Wananchi Bumbuli
Makamba amekanusha madai hayo alipoulizwa na waandishi wa habari waliopiga kambi ofisini kwake jijini Dar es Salaam kutaka kupata maoni yake baada ya kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM(NEC) Taifa, kilichoketi Julai 28, 2025 kutomteua kwenye kinyang’anyiro cha ubunge ndani ya CCM jimboni kwake Bumbuli, wilaya ya Lushoto mkoani Tanga.







