Warsha za ufundaji wa fanani, watunzi na wahakiki, uwekezaji wa kutosha, uhamasishaji na usimamizi bora vitasaidia sana katika kuimarisha ufahamu wa kitaalamu na utambuzi mpana katika utunzi, uwasilishaji na uhakiki wa kazi za fasihi, kwa kuzingatia kunga zake.