
Zitto Kabwe: Taasisi za Kimataifa Zina Nguvu Sana Tanzania Kuliko Watanzania
Kiongozi huyo wa kisiasa anasema hilo limejidhihirisha kwenye hatua ya Serikali kubatilisha marufuku yake ya awali iliyokuwa inawazuia wasichana wanaopata ujauzito wakiwa shuleni kuendelea na masomo baada ya kujifungua, akidai hatua hiyo imetokana na shinikizo kutoka Benki ya Dunia.