The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on April 20, 2024. Register Here

Search
Close this search box.

Fahamu Kuhusu Tausi, Mfumo Mpya wa Ukusanyaji Mapato Serikalini

Unatajwa kuongeza ufanisi kwenye ukusanyaji mapato na kuepusha upotevu.

subscribe to our newsletter!

Dodoma. Mkurugenzi wa TEHAMA, Ofisi ya Rais TAMISEMI mkoani Dodoma Erick Kitali, ameeleza kwamba mfumo mpya wa ukusanyaji wa mapato ya ndani ya halmashauri ujulikanao kama Tausi utasaidia kupunguza urasimu uliokuwepo hapo awali kwenye ukusanyaji wa mapato.

Kitali alitoa tathmini hiyo wakati wa mahojiano maalum na The Chanzo yaliyofanyika ofisini kwake mjini hapa hivi karibuni kuhusu mfumo huo unaotajwa kubuniwa na wataalam wa ndani ya nchi.

Ukipewa jina la ndege huyo mzuri anayepatikana nchini Tanzania, Tausi umebuniwa baina ya kubainika uwepo wa changamoto mbalimbali kwenye mfumo uliokuwa unatumika hapo awali, ikiwa ni pamoja na uzoefu wa mlipa kodi.

“Mfumo huu utasaidia kupunguza muda, kuondoa urasimu uliokuwepo kwa baadhi ya sehemu,” Kitali alisema kwenye mahojiano hayo. “Na sehemu nyingine tulikuwa tunaambiwa kwamba kuna rushwa tumepunguza kwa sababu hukutani moja kwa moja na mwananchi.”

SOMA ZAIDI: Nini Kifanyike Kuboresha Mfumo wa Kodi 2023?

Pamoja na mambo mengine, mfumo wa Tausi humsaidia mteja kufanya malipo kwa kutumia VISA, MasterCard na namba ya malipo kutoka Mfumo wa Malipo wa Kielektroniki wa Serikali (GePG).

Mfumo huo pia humsaidia mteja kujihudumia mwenyewe, hali ambayo haimlazimu tena kwenda ofisi za halmashauri kuomba, au kulipia, tozo, ushuru, leseni, faini au vibali mbalimbali badala yake anaweza kufanya mwenyewe kupitia dirisha la mteja, au Taxpayer Portal

Kabla ya ujio wa mfumo huo, Serikali ilikuwa inatumia mfumo wa LGRCIS, au Local Government Revenue Collection Information System, ambao Kitali alisema kwenye mahojiano yake na The Chanzo kwamba ulipaswa ubadilishwe ili kuendana na kasi ya mabadiliko ya kiteknolojia.

Akizungumzia kuhusu namna wananchi walivyoupokea mfumo huo mpya, Kitali alisema mpaka sasa muitikio ni mkubwa.

“Kwa sababu wananchi walikuwa wanapata changamoto ya kupoteza muda mwingi sana kwenda kufuatilia huduma,” alisema. “Ule urahisi wa kufanya malipo mbalimbali ya Serikali umesaidia wananchi kuwa na muitikio mkubwa.” 

“Umeongeza uaminifu kwa wananchi kwa Serikali yao kwa sababu wana uhakika na fedha wanayoilipa inakwenda moja kwa moja kwenye Serikali,” aliongeza Kitali. “Pia, mfumo huu umesaidia fedha zinazokusanywa [na halmashauri] zinapelekwa benki kwa wakati.”

SOMA ZAIDI: Aidan Eyakuze: Ni Wajibu wa Wananchi Kusimamia Uwazi, Uwajibikaji Serikalini

Kitali alisema kwamba faida nyengine kwa upande wa Serikali inayotokana na matumizi ya mfumo huo ni kwenye eneo zima la usimamizi wa mashine za ukusanyaji wa mapato, yaani POS. 

“Tulikuwa tuna changamoto, saa nyingine usijue zipo ngapi,” alisema afisa huyo. “Lakini sasa hivi, kwa kutumia mfumo huu, tumeboresha hilo eneo [na] kuhakikisha kwamba POS zote ambazo zipo kwenye halmashauri tunajua zipo ngapi, zinatumiwa na nani na zimekusanya kwa kipindi gani.”

Kitali alisema kwamba matarajio ya Serikali kwa sasa ni kuongeza ubora wa huduma kwa wananchi, akisema kwamba huduma bora husaidia kuongeza mapato serikalini. 

“Wito wetu kwa wananchi ni kwamba tunaomba waendelea kuutumia mfumo huu na panapotokea changamoto yoyote basi watujulishe,” alisema mtaalamu huyo. 

“Na uzuri tulichokifanya, watalaam wetu wa halmshauri wamefundishwa [kuutumia huu mfumo], maafisa bishara [na] maafisa fedha wanaufahamu mpaka ngazi ya mkoa,” aliongeza Kitali.

Jackline Kuwanda ni mwandishi wa habari wa The Chanzo anapatikana mkoani Dodoma unaweza kumpata kupitia jackline@thechanzo.com

Digital Freedom and Innovation Day
The Chanzo is hosting Digital Freedom and Innovation Day on Saturday April 20, 2024 at Makumbusho ya Taifa.

Register to secure your spot

15 Responses

  1. Kwa system hiyo ,mfumo utasaidia Sana mwananchi ,kuondokana na changamoto za rushwa,kufaidisha mmtu binafsi kuliko serikali ,na kupunguza kupoteza mda ,/kutumia mda mrefu kwa kitu kidogo

  2. Ila kuna changamoto katika upande wa leseni za biashara kwani kuna baadhi ya shughuli hakuna kwa mfano mimi nafanya kazi za kupakia na kushusha cement ..hii kazi haipo kwenye mfumo. Ningeomba kiongezwe kipengele cha kuandika aina ya biashara kwa mtu mwenyewe .kwa sababu biashara ni nyingi na ndio maana hata kwenu imekua ngumu kuainisha zote… hii itasaidia kumpa uhuru muombaji.. kuna waombaji wengi wanashindwa kuomba kwa sababu aina za biashara zao hazipo kwenye mfumo

  3. Mfumo ni mzuri,utaokoa muda ila badala yake uko chini sana yaani jambo moja linachukua zaidi ya masaa manne kwa mfano leseni ya biashara kisha ukikamisha na kutuma inachukua zaidi ya siku moja kupata namba ya malipo sasa inakatisha tamaa, kwa hiyo hapo hamko vizuri.

  4. Nimejisajili ila mpaka sasa sijapata namba ya malipo, naona bado ni usumbufu, jaribuni kuboresha uwe rahisi zaidi tuokoe muda

    1. Aiseee.. inapoteza muda na ni usumbufu wa hali ya juu.. toka asubuhi hadi sasa sijapata contro number licha ya kusajili. Mtu unahisi labda umekosea sehem.. unarudia lakini wapi. Tupeni ufafanuzi mzuri maana jamaa wakija kudai leseni na uwaambie mfumo unasumbua sizani kama watakuelewa. Ni kero kwa kweli

  5. Aiseee.. inapoteza muda na ni usumbufu wa hali ya juu.. toka asubuhi hadi sasa sijapata contro number licha ya kusajili. Mtu unahisi labda umekosea sehem.. unarudia lakini wapi. Tupeni ufafanuzi mzuri maana jamaa wakija kudai leseni na uwaambie mfumo unasumbua sizani kama watakuelewa. Ni kero kwa kweli

  6. tunaomba msaada maana sijafanikiwa toka nimeanza tumia hii program na siku zina dhidi kuisha na hili tatizo sidhani kama litatatulika mapema tunaomba njia mbadala ya kulipia leseni pls

  7. Mifumo imekaa kipigaji…. mifumo kila kona kuna matatizo unajisajili mwisho wa siku hupati control number na badala yake unapewa taarifa ya BAD CREDIDENTIAL,BAD GATEWAY yaani mama kutatua swala la Rushwa afukuze baadhi ya wapigaji kwenye maofisi……

    Very poor Customer Care…. mnapo anzisha kitu wekeni na dawati la huduma kwa wateja

  8. mi kwa ushauri wangu naona mtandao unasumbua hata katika kujaza kwenye system katika kupata lessen inabidi waboreshe mtandao uwe vizuri maana mtu hata wiki zima hata ukijanza haitumi hizo utp

  9. Huo mfumo ni kupotezeana muda tu….jambo la kufanya ndani ya nusu saa….unafanya wiki nzim!!!!. Afu huko wilayani kuna maafisa wanaomba wapewe elf15 ili wakusaidie upate leseni. Shame!!!

  10. Mimi kama mkurugenzi wa kampuni nagombana na mfanyakazi anayeshughulikia leseni, na mhasibu na wengine pale wanaposhindwa kupata leseni eti mfumo hautoi ctrl namba kwa urahisi. Sasa hata kulipia leseni ni kero. Kwani hii mifumo inaharakisha biashara au kinyume. Si mfanye tafiti kabla ya kuanyika mapungufu ya mfumo mpya?

  11. Kwa upande wangu nafikiri nitakuwa tofauti kidogo, issue ya control number sio TAUSIA tu hata ukienda TRA utakutana na shida hiyo kikubwa ni watalamu wa sehemu zote waweze kuhakikisha Control number zinatoka especially watu wa GePG maana ndio wahusika wakubwa wa control number na halmashauri maafisa biashara waharakishe kufanya mapitio ya maombi . mimi nilipata leseni ndani ya masaa 2 tu pale kinondoni manispaa

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *