
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Yatoa Ufafanuzi Takwimu za Wapiga Kura
Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye pia ni Katibu wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi(INEC), Ramadhani Kailima amesema kuwa hakuna takwimu za wapiga kura zilizoongezeka kwenye daftari la kudumu la wapiga kura kama ilivyolinganishwa na baadhi ya watu na takwimu za makadirio ya wapiga kura kwa mujibu wa Sensa.








