Nini Maana ya Ukimya wa Afrika Kwenye Mgogoro wa Urusi na Ukraine?
Baadhi ya wadau wangetegemea nchi za Afrika ziitete Ukraine ambayo katika mgogoro huu ni taifa dhaifu kuliko hasimu wake Urusi. Mantiki hii inatokana na busara kuwa nchi zisizo na nguvu zinateteana.