
Balozi wa Ukraine Nchini Kenya Kukutana na Raia wa Ukraine Waliokwama Zanzibar
Ukraine na Zanzibar wanafanya mazungumzo ya kuwasafirisha raia hao wapatao 900 mpaka nchini Poland ambayo kwa sasa inapokea wakimbizi wengi kutoka Ukraine.

Ukraine na Zanzibar wanafanya mazungumzo ya kuwasafirisha raia hao wapatao 900 mpaka nchini Poland ambayo kwa sasa inapokea wakimbizi wengi kutoka Ukraine.

Drone moja inaripotiwa kuwa na uwezo wa kutafiti shamba moja la mpunga lenye ukubwa wa ekari 30 kwa muda wa dakika 20 tu. Picha zinazochukuliwa zinaweza kuchakatwa ndani ya muda huo huo ili kugundua na kutengeneza ramani ya mazalia ya mbu.

Video za ndugu hao zikiwaonesha wakiimba nyimbo mbalimbali za wasanii mashuhuri kutoka nchini India zimekuwa zikisambaa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii hivi karibuni, hususan TikTok na Instagram na kuweza kujivutia mashabiki wengi kutoka sehemu mbalimbali za dunia.

Ripoti hiyo iliyochapishwa Februari 10, 2022, inatoa mapendekezo sita ambayo wanamazingira wanaamini kwamba kama yatatekelezwa vizuri yataifanya EAC kuwa katika viwango vya kimataifa juu ya ulindaji wa mazingira.

The Chanzo inazungumza na mwanaharakati Tito Magoti kupata mtazamo wake wa haki za binadamu chini ya utawala wa Rais Samia Suluhu Hassan na mapendekezo yake ya namna ya kuboresha mfumo wa haki jinai nchini Tanzania.

Mamlaka hiyo ya uhifadhi wa wanyamapori yadai wakulima hao walivamia eneo la hifadhi, madai ambayo wakulima na mamalaka nyengine za Serikali zinapingana nayo.

Kwa mujibu wa NBS, baadhi ya vyakula vilivyoripotiwa kupanda bei ni pamoja na mchele, mahindi, unga wa ngano, unga wa mahindi, mboga mboga, viazi vitamu, viazi mviringo, ndizi na maharage.

Hii ni kwa kipindi cha Julai mpaka Septemba 2021 tu.

Wafanyakazi hao wanamlalamikia Waziri wa Kilimo Hussein Bashe ambaye alikuwa Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo wakati wafanyakazi hao kutoka idara mbalimbali na maeneo mbalimbali ya nchi walikuwa wakiitumikia kampuni hiyo.

Kampuni hiyo ya simu imehusisha anguko hilo na tozo zinazotozwa kwa Watanzania pale wanapofanya miamala kwa kutumia simu za mkononi.